Marekani yaendeleza mashambulizi ya anga Iraq,huku Uingereza ikiahidi kutoa msaada wa kijeshi kwa Wakrudi.
Marekani inaendelea kufanya mashambulizi ya anga kaskazini
mwa Iraq, lengo la Marekani kuendeleza
mashambulizi ya anga Iraq ni kupambana na kundi la wapiganaji wa kiislam
linalofahamika kama Jihadi .
Marekani imezidi kuongeza wanajeshi ili kutoa msaada kwa Wakrudi
waishio mji wa Erbil ambao wako kwenye mapambano dhidi ya wapiganaji hao wa
kiislam.
![]() |
Wapiganaji wa jeshi la Wakrudi |
Licha ya hivyo bado kundi la wapiganaji wa kiislam wanazidi
kuimarisha ngome yao katika eneo hilo,pia kuiteka ngome kubwa ya Iraq katika
mji wa Mosul.
Jeshi la Marekani limesema limefanya mashambulizi dhidi ya
wapiganaji wa Sunni waliokuwa wamejificha katika milima iliyo eneo la wakimbizi
la Yazid ili kuzuia wapiganaji hao wasiendelee kufanya njama za mashambulizi.
Licha ya Marekani kutoa msaada kwa Wakrudi, Uingereza nayo
imeahidi kuendelea kutoa misaada ya kibinadamu kwa Wakrudi.Ofisa wazamani wa
mambo ya kigeni wa Uingereza Alistair Burt ame
Mgogoro baina ya Wakrudi na kundi la wapiganaji wa Kiislam
umesababishwa na tofauti za kidini ambapo kundi hilo la Jihad huwalazimisha
maelfu ya watu waishio nchini Iraq kufuata
itikadi za dini ya kiislam .
Nae papa Francis ametoa wito kwa dunia kukomesha uhalifu huo
unaoendelea kufanywa nchini Iraq na kuwataka watu waache kubaguana kutokana na
tofauti za kidini,alisema maneno hayo wakati wa ibada iliyofanyika siku ya jumapili iliyo pita.
No comments:
Post a Comment