Thursday, 28 August 2014

Spika wa Bunge la Niger atoroka baada ya kukumbwa na kashfa ya kuuza watoto nje ya nchi



Spika wa bunge la Niger Hama Amadou ametoroka nchini kwao baada ya kamati ya bunge hilo kuafikia kukamatwa kwake kuhusiana na kashfa ya kuwauza watoto nje ya nchi.
Licha ya kashfa hiyo mtuhumiwa Hama Amadou alidai kuwa kashfa hiyo si ya kweli na imechochewa na tofauti za kisiasa hasa katika kipindi hiki alichotangaza nia yake ya kugombea kiti cha urais mwaka 2016.
Spika wa bunge la Niger Hama Amadou
Aidha mke  wa pili spika huyo na watu wengine 16 walikamatwa mwezi Juni baada ya kutuhumiwa kuwauza watoto wachanga kusini mashariki mwa Nigeria,watoto hao huuzwa kwa gharama kubwa yapata maelfu ya dola za kimarekani kwa kila mtoto.
Vyombo vya habari nchini Niger vimeeleza kuwa kesi hiyo imetoa fursa tosha kwa chama tawala kumuondoa Bwana Amadou kutoka katika chama hicho.
Kamati kuu ya bunge la Taifa ambalo linajumuisha naibu spika na wakuu wengine walikutana jumatano na kukubaliana kuwa polisi wanaweza kumkamata na kumhoji bwana Amadou kuhusiana na tuhuma hizo.
Inadaiwa hadi sasa watoto 30 wameuzwa katika hii inayohusishwa na utengenezwaji wa stakabadhi bandia na kubadili vyeti vya kuzaliwa vya watoto waliouzwa.  

No comments: