Thursday 17 December 2015

Shirika la OXFAM lapania kuwezesha vijana

Shirika lisilo la kiserikali la OXFAM kwa kushirikiana na taasisi tano za vijana nchini(DARUSO,TYDC,YouthCAN,YOUNG FEMINIST FORUM na NGAO YOUTH ) limepania kuwainua vijana walio chini ya umri wa miaka 24 kiuchumi na kutimiza ndoto zao kupitia mradi wao wa MSAFARA.
Vijana wa Msafara wakielekea Ifakara
Hivi sasa mradi wa Msafara upo kwenye majaribio ambapo wameshafanya matamasha mawili Dar Es Salaam na Morogoro.Jijini Dar Es Salaam tamasha lilifanyika tarehe 4 disemba kwenye ukumbi wa Nkurumah, lilihudhuriwa na vijana zaidi ya 500 kutoka sehemu mbalimbali
vijana waliohudhuria tamasha la Msafara kwenye ukumbi wa Nkurumah,jijini Dsm
,na tamasha la mkoani Morogoro lilifanyika kwenye Uwanja wa Taifa uliopo Ifakara wilaya ya Kilombero tarehe 12 disemba mwaka huu.
Mradi wa Msafara unatarajiwa kuanza rasmi Januari mwakani,unatarajiwa kuzunguka Tanzania nzima na kuchagua vijana wenye vipaji,ndoto na mawazo yatakayobadilisha maisha yao na Taifa kiujumla.
Lengo la Msafara ni kuwawezesha vijana kuwa wabunifu,kuwahamasisha ili kuzifikia ndoto zao na kuwatengenezea mazingira rafiki yatakayo wawezesha wao kujiajiri wenyewe.
 Mwenyekiti wa Msafara Bw. James Isdore,aliwataka vijana kuitumia fursa hii ili kujitengenezea mazingira mazuri ya wao kujiajiri na kuwezeshwa kiuchumi.
Mwenyekiti wa Msafara(wa pili kutoka kushoto) James Isdore akiongea na Waandishi wa Habari Dsm

"Vijana inabidi wajifunze kuzitumia fursa kama hizi,mradi wa Msafara una lengo la kuweka ubunifu wa vijana wazi ili kuwavutia wengine waweze kufanya zaidi na kuimarisha ubunifu wao,pia tunahamasisha vijana kuchukua hatua na kufanya zaidi basada ya kujifunza kutoka kwa wenzao pamoja na kuziibua changamoto za mafanikio ya kimaisha na jinsi ya kukabiliana nazo." Alisema Isdore     

No comments: