Saturday 11 October 2014

Mlipuko wa Ebola waipa hofu nchi ya Morocco

Vyombo vya habari nchini Morocco vinasema kuwa serikali ya taifa hilo imeomba kinyang'anyiro cha kuwania kombe la klabu bingwa barani Afrika cha mwaka ujao kuahirishwa kutokana na mlipuko wa ugonjwa wa ebola.
Maiti ya Mgonjwa wa Ebola ikienda kuhifadhiwa na wahudumu
Hatua hiyo iliafikiwa kutokana na pendekezo la wizara ya afya ambayo inataka kuyazuia mataifa ambayo yameathiriwa na ugonjwa huo.
Maafisa nchini Moroco watafanya mazungumzo kuhusu ombi hilo na waandalizi wake ambacho ni chama cha kandanda barani afrika CAF wiki ijayo.
Mechi za kufuzu zinazoshirikisha nchi mbili ambazo zimeathiriwa na ugonjwa wa ebola ambazo ni Guinea na Liberia tayari zimehamishwa ikiwamo mechi ambayo ilitarajiwa kuchezwa leo .

No comments: