Sunday, 10 August 2014

Mgogoro wa Palestina na Israel,umeshindikana


Kiongozi wa juu wa kundi la Hamas amesema kuwa kuna uwezekano mdogo wa mazungumzo ya kuleta amani Gaza kufanikiwa kutatua mgogoro kutokana nahali ya kutoelewana kwa wajumbe waliohudhuria mkutano huo mjini Cairo.

Kiongozi huyo aliyasema hayo katika mkutano mjini Cairo ambao ulihusisha wajumbe mbali mbali toka Misri,Ezzat AL-rishq ambaye ni mmoja kati ya wajumbe kutoka Palestina  ambaye aliteuliwa katika mkutano huo aliliambia shirika la habari la AFP kuwa nafasi ya mapatano kati yao ni ndogo sana.

Naye waziri mkuu wa Israel,Benjamin Netanyahu amesema wawakilishi wake waliondoka Misri tangu ijumaa na hawatarejea ikiwa maroketi yataendelea kurushwa Israel na wapalestina.

Hadi sasa hali ya Gaza si shwari,maafisa mjini Gaza wanasema hivi leo kuna mwanamke ameuawa na watu wengine nane wa familia yake wamejeruhiwa baada ya kombora kutoka Israel kuipiga nyumba yao iliyo kusini mwa mji wa Bani Suheila.

Mtu mwengine mmoja aliuawa katika kambi ya wakimbizi wa kipalestina ya Jabaliya.Hadi sasa wapalestina 1,900 wamepoteza maisha kati ya hao robo ya idadi yao walikuwa watoto.

No comments: