Sunday, 10 August 2014

Davido:Skendo hazinitishi tena



Msanii maarufu kutoka nchini Nigeria David Adeleke Adedeji(Davido) anayetamba hivi sasa na nyimbo ya SKELEWU,TCHELETE aliye shirikisha kundi matata toka nchini South Afrika maarufu kama Mafikizolo hivi karibu alifunguka na kusema kuwa kutokana na umaarufu alio nao haogopi skendo tena.

Licha ya nyimbo hizo zinazozidi kumpa umaarufu bado msanii huyu anaongoza kwa kuwa na uwezo wa  kufanya show 19 kwa mwezi kutokana na mashabiki aliofanikiwa kuwa nao Afrika na nje ya Afrika.

Davido amepata tuzo tofauti kama BET International Award,MTV MAMA,Kora Award,Channel O Music  Video Award,Ghana Music Award,Nigeria Music Award n.k zilimfanya azidi kuwa kivutio kwa wadau wa muziki duniani.
Davido

Davido alisema maneno hayo kwamba haogopi tena skendo zinazo sababishwa na umaarufu aliokuwa nao sasa katika mahojiano yaliyofanywa na chombo cha habari nchini Nigeria kinachofahamika kwa jina la Nigeriacamera.

Hivi karibuni msanii huyu alipata skendo ya kumnyanyapaa msanii mwenzake Wizkid wakati akifanya show nchini Marekani.

No comments: