Thursday 24 May 2018

MEYA MWITA KUNOGESHA FAINALI ZA PAMBANO LA NGUMI KESHO

MPAMBANO wa shindano la kombe la ngumi la Mstahiki Meya wa jiji la Dar es Salaam, Isaya Mwita limeendelea kushika kasi kabla ya kuingia fainali hapo kesho.

Jula ya  mabondia 36 wataingia uliongoni leo kupimana nguvu katika uwanja wa ndani wa Taifa kutafuta mabondia 20 watakao ingia kwenye fainali hapo kesho.


Mchuano huo wa aina yake hapo kesho utashuhudiwa na Meya Mwita na wananchi wa jijini hapa ambapo mshindi wa kwanza atapata zawadi ya kombe,huku mshindi wa pili kwa kila uzito atapata medali za dhahabu.

Aidha mshindi wa tatu kwa kila uzito atapatiwa zawadi ya medali za fedha ambapo zawadi hizo zitatolewa kwa washindi na Meya Mwita.

Mwisho.

Imetolewa leo ,Mei 24 na Christina Mwagala, Afisa habari Ofisi ya Meya wa jiji.

No comments: