Thursday 24 May 2018

KOREA KASKAZINI YAIONYESHEA UBABE MAREKANI, YASEMA HAIWEZI KUACHANA NA MPANGO WA NYUKLIA


Korea Kaskazini imesema haiwezi kuibembeleza Marekani kuhusu mazungumzo baina ya mataifa hayo mawili yanayotarajiwa kufanyika mwezi Juni mwaka huu.

Kiongozi mwandamizi wa Korea Kaskazini, Choe Son-hui amenukuliwa akimtuhumu Makamu wa Rais wa Marekani, Mike Pence kwamba ni mjinga, huku akitishia kuwa iwapo mazungumzo hayo yasipofanyika kutakuwepo maonyesho ya ubabe wa nyuklia.


Siku za hivi karibuni pande hizo mbili zimeonya kwamba mkutano huo unaweza kuahirishwa au kufutwa kabisa.

Korea Kaskazini ilisema itafikiria tena iwapo itahudhuria mkutano ikiwa Marekani itaendelea kusisitiza kuwa iachane na mpango wa silaha za nyuklia.

No comments: